Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:127-146 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:127-146 in Biblia ya Kiswahili

127 Hakika ninazipenda amri zako kuliko dhahabu, naam, kuliko dhahabu safi.
128 Hivyo ninayafuata maagizo yako yote kwa makini, na ninachukia kila njia ya uongo. PE.
129 Sheria zako ni za ajabu, ndiyo sababu ninazitii.
130 Ufafanuzi wa maneno yako huleta nuru; na kumpa ufahamu mjinga.
131 Ninafungua kinywa changu na kutweta, maana ninazitamani amri zako.
132 Unigeukie na unihurumie, kama ufanyavyo siku zote kwa wale walipendao jina lako.
133 Uziongoze hatua zangu kwa neno lako; usiruhusu dhambi yeyote initawale.
134 Unikomboe dhidi ya wanadamu waonevu ili niyatii maagizo yako.
135 Uso wako umwangazie mtumishi wako, na unifundishe sheria zako.
136 Mito ya machozi yatiririka kutoka machoni pangu kwa sababu watu hawaitii sheria yako. TSADHE.
137 Wewe ni mwenye haki, Yahwe, na amri zako ni haki.
138 Umezipa amri za agano lako haki na uaminifu.
139 Hasira imeniangamiza kwa sababu adui zangu husahau maneno yako.
140 Neno lako limepimwa sana, naye mtumishi wako analipenda.
141 Sina umuhimu na ninadharauliwa, lakini bado siyasahau maagizo yako.
142 Hukumu yako ni ya haki milele, na sheria yako ni ya kuaminika.
143 Japo dhiki na taabu vimenipata, amri zako bado ni furaha yangu.
144 Amri za agano lako ni za haki milele; unipe uelewa ili niweze kuishi. QOPH.
145 Nililia kwa moyo wangu wote, “Unijibu, Yahwe, nitazishika sheria zako.
146 Ninakuita wewe; uniokoe, nami nitazitii amri za agano lako.”
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili