125 Mimi ni mtumishi wako; unipe uelewa ili niweze kuzijua amri za agano lako.
126 Ni wakati wa Yahwe kutenda, kwa maana watu wamevunja sheria yako.
127 Hakika ninazipenda amri zako kuliko dhahabu, naam, kuliko dhahabu safi.
128 Hivyo ninayafuata maagizo yako yote kwa makini, na ninachukia kila njia ya uongo. PE.
129 Sheria zako ni za ajabu, ndiyo sababu ninazitii.
130 Ufafanuzi wa maneno yako huleta nuru; na kumpa ufahamu mjinga.
131 Ninafungua kinywa changu na kutweta, maana ninazitamani amri zako.
132 Unigeukie na unihurumie, kama ufanyavyo siku zote kwa wale walipendao jina lako.
133 Uziongoze hatua zangu kwa neno lako; usiruhusu dhambi yeyote initawale.
134 Unikomboe dhidi ya wanadamu waonevu ili niyatii maagizo yako.
135 Uso wako umwangazie mtumishi wako, na unifundishe sheria zako.
136 Mito ya machozi yatiririka kutoka machoni pangu kwa sababu watu hawaitii sheria yako. TSADHE.
137 Wewe ni mwenye haki, Yahwe, na amri zako ni haki.
138 Umezipa amri za agano lako haki na uaminifu.
139 Hasira imeniangamiza kwa sababu adui zangu husahau maneno yako.
140 Neno lako limepimwa sana, naye mtumishi wako analipenda.
141 Sina umuhimu na ninadharauliwa, lakini bado siyasahau maagizo yako.