Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:122-133 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:122-133 in Biblia ya Kiswahili

122 Uwe mdhamini wa ustawi wa mtumishi wako; usiwaache wenye kiburi wanionee.
123 Macho yangu yanachoka kwa kuusubiri wokovu wako na neno lako la haki.
124 Mwoneshe mtumishi wako uaminifu wa agano lako, na unifundishe sheria zako.
125 Mimi ni mtumishi wako; unipe uelewa ili niweze kuzijua amri za agano lako.
126 Ni wakati wa Yahwe kutenda, kwa maana watu wamevunja sheria yako.
127 Hakika ninazipenda amri zako kuliko dhahabu, naam, kuliko dhahabu safi.
128 Hivyo ninayafuata maagizo yako yote kwa makini, na ninachukia kila njia ya uongo. PE.
129 Sheria zako ni za ajabu, ndiyo sababu ninazitii.
130 Ufafanuzi wa maneno yako huleta nuru; na kumpa ufahamu mjinga.
131 Ninafungua kinywa changu na kutweta, maana ninazitamani amri zako.
132 Unigeukie na unihurumie, kama ufanyavyo siku zote kwa wale walipendao jina lako.
133 Uziongoze hatua zangu kwa neno lako; usiruhusu dhambi yeyote initawale.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili