Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:121-128 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:121-128 in Biblia ya Kiswahili

121 Ninafanya kilicho sahihi na haki; usiniache kwa watesi wangu.
122 Uwe mdhamini wa ustawi wa mtumishi wako; usiwaache wenye kiburi wanionee.
123 Macho yangu yanachoka kwa kuusubiri wokovu wako na neno lako la haki.
124 Mwoneshe mtumishi wako uaminifu wa agano lako, na unifundishe sheria zako.
125 Mimi ni mtumishi wako; unipe uelewa ili niweze kuzijua amri za agano lako.
126 Ni wakati wa Yahwe kutenda, kwa maana watu wamevunja sheria yako.
127 Hakika ninazipenda amri zako kuliko dhahabu, naam, kuliko dhahabu safi.
128 Hivyo ninayafuata maagizo yako yote kwa makini, na ninachukia kila njia ya uongo. PE.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili