Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:113-134 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:113-134 in Biblia ya Kiswahili

113 Ninawachukia watu wa kusita-sita, lakini naipenda sheria yako.
114 Wewe ni ficho langu na ngao yangu; nalingoja neno lako.
115 Ondokeni kwangu, ninyi mtendao uovu, ili niweze kuzitii amri za Mungu wangu.
116 Uniwezeshe kwa neno lako ili niweze kuishi na nisiaibike na matumaini yangu.
117 Unisaidie, nami nitakuwa salama; siki zote nitazitafakari sheria zako.
118 Wewe huwakataa wale wote wapoteao mbali na sheria zako, maana watu hao ni wadanganyifu na si wakuaminika.
119 Wewe huwaondoa waovu wa nchi kama takataka; kwa hiyo ninazipenda amri zako thabiti.
120 Mwili wangu hutetemeka kwa hofu yako, na ninaziogopa amri za haki yako. AYIN.
121 Ninafanya kilicho sahihi na haki; usiniache kwa watesi wangu.
122 Uwe mdhamini wa ustawi wa mtumishi wako; usiwaache wenye kiburi wanionee.
123 Macho yangu yanachoka kwa kuusubiri wokovu wako na neno lako la haki.
124 Mwoneshe mtumishi wako uaminifu wa agano lako, na unifundishe sheria zako.
125 Mimi ni mtumishi wako; unipe uelewa ili niweze kuzijua amri za agano lako.
126 Ni wakati wa Yahwe kutenda, kwa maana watu wamevunja sheria yako.
127 Hakika ninazipenda amri zako kuliko dhahabu, naam, kuliko dhahabu safi.
128 Hivyo ninayafuata maagizo yako yote kwa makini, na ninachukia kila njia ya uongo. PE.
129 Sheria zako ni za ajabu, ndiyo sababu ninazitii.
130 Ufafanuzi wa maneno yako huleta nuru; na kumpa ufahamu mjinga.
131 Ninafungua kinywa changu na kutweta, maana ninazitamani amri zako.
132 Unigeukie na unihurumie, kama ufanyavyo siku zote kwa wale walipendao jina lako.
133 Uziongoze hatua zangu kwa neno lako; usiruhusu dhambi yeyote initawale.
134 Unikomboe dhidi ya wanadamu waonevu ili niyatii maagizo yako.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili