Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:105-114 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:105-114 in Biblia ya Kiswahili

105 Neno lako ni taa ya mguu miguu yangu na mwanga wa njia yangu.
106 Nimeapa na nimethibitisha, kuwa nitazitii amri za haki yako.
107 Nimeteswa sana; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika neno lako.
108 Yahwe, tafadhali pokea dhabihu yangu ya hiari ya kinywa changu, na unifundishe amri zako za haki.
109 Uhai wangu ziku zote uko mkononi mwangu, lakini bado sisahau sheria yako.
110 Waovu wamenitegea mtego, lakini sijapotea mbali na maagizo yako.
111 Nimezifanya amri za agano lako kama urithi wangu milele, maana hizo ni furaha ya moyo wangu.
112 Moyo wangu umewekwa kuzitii sheria zako milele mpaka mwisho kabisa. SAMEKH.
113 Ninawachukia watu wa kusita-sita, lakini naipenda sheria yako.
114 Wewe ni ficho langu na ngao yangu; nalingoja neno lako.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili