Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 8:9-27 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 8:9-27 in Biblia ya Kiswahili

9 Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
10 Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
12 Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
13 Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
14 Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
15 Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
16 Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
17 Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
18 Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
20 Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
21 katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
22 Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
23 Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
24 Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
25 Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
26 Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
27 Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
Mithali 8 in Biblia ya Kiswahili