Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 8:5-22 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 8:5-22 in Biblia ya Kiswahili

5 Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
6 Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
7 Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
8 Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
9 Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
10 Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
12 Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
13 Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
14 Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
15 Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
16 Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
17 Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
18 Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
20 Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
21 katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
22 Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
Mithali 8 in Biblia ya Kiswahili