Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 8:3-15 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 8:3-15 in Biblia ya Kiswahili

3 Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
4 Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
5 Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
6 Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
7 Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
8 Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
9 Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
10 Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
12 Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
13 Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
14 Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
15 Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
Mithali 8 in Biblia ya Kiswahili