Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 30:7-23 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 30:7-23 in Biblia ya Kiswahili

7 Vitu viwili ninakuomba, usivikatalie kwangu kabla sijafa:
8 Majivuno na uongo viweke mbali nami. Usinipe umasikini wala utajiri, nipe tu chakula ninachohitaji.
9 Maana nikipata vingi zaidi, nitakukana wewe na kusema, “Yehova ni nani?” Au kama nitakuwa masikini, nitaiba na kukufuru jina la Mungu wangu.
10 Usimkashifu mtumwa mbele ya bwana wake, au atakulaani na utapata hatia.
11 Kizazi ambacho kinachomlaa baba yao na hakimbariki mama yao,
12 kizazi hicho ni safi katika macho yao wenyewe, lakini hawajaoshwa uchafu wao.
13 Hicho ni kizazi- jinsi gani macho yao yanakiburi na kope zao zimeinuka juu! -
14 kuna kizazi ambacho meno yao ni upanga, na mifupa ya taya zao ni visu, ili waweze kumrarua masikini wamtoe duniani na mhitaji atoke miongoni mwa wanadamu.
15 Ruba anamabinti wawili, “Toa na Toa” wanalia. Kuna vitu vitatu ambavyo havitosheki, vinne ambavyo havisememi, “Inatosha”:
16 Kuzimu, tumbo tasa, nchi yenye kiu kwa maji, na moto usiosema, “Inatosha.”
17 Jicho ambalo linamdhihaki baba na kudharau utii kwa mama, macho yake yatadonolewa na kunguru wa bondeni, na ataliwa na tai.
18 Kuna vitu vitatu ambavyo vinanishangaza, vinne ambavyo sivifahamu:
19 njia ya tai angani; njia ya nyoka juu ya mwamba; njia ya meli kwenye moyo wa bahari; na njia ya mtu pamoja mwanake kijana.
20 Hii ni njia ya mzinzi- anakula na kufuta kinywa chake na kusema, “sijafanya ubaya wowote.”
21 Chini ya vitu vitatu dunia hutetemeka na vinne haiwezi kuvivumilia:
22 mtumwa anapokuwa mfalme; mpumbavu anaposhiba vyakula;
23 mwanamke anayechukiwa anapoolewa; kijakazi anapochukua nafasi ya mkuu wake.
Mithali 30 in Biblia ya Kiswahili