Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 30:2-15 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 30:2-15 in Biblia ya Kiswahili

2 Hakika nipo kama mnyama kuliko mwanadamu na sina ufahamu wa wanadamu.
3 Sijajifunza hekima, wala sina maarifa ya Mtakatifu.
4 Je ni nani amekwenda juu mbinguni na kurudi chini? Je ni nani aliyekusanya upepo kwenye mikono yake? Je ni nani aliyekusanya maji kwenye kanzu? Je ni nani aliyeziimarisha ncha za dunia yote? Jina lake ni nani, na jina la mtoto wake ni nani? Hakika unajua!
5 Kila neno la Mungu limejaribiwa, yeye ni ngao kwa wale wanaokimbilia kwake.
6 Usiyaongezee maneno haya, au atakukemea, na utathibitishwa kuwa mwongo.
7 Vitu viwili ninakuomba, usivikatalie kwangu kabla sijafa:
8 Majivuno na uongo viweke mbali nami. Usinipe umasikini wala utajiri, nipe tu chakula ninachohitaji.
9 Maana nikipata vingi zaidi, nitakukana wewe na kusema, “Yehova ni nani?” Au kama nitakuwa masikini, nitaiba na kukufuru jina la Mungu wangu.
10 Usimkashifu mtumwa mbele ya bwana wake, au atakulaani na utapata hatia.
11 Kizazi ambacho kinachomlaa baba yao na hakimbariki mama yao,
12 kizazi hicho ni safi katika macho yao wenyewe, lakini hawajaoshwa uchafu wao.
13 Hicho ni kizazi- jinsi gani macho yao yanakiburi na kope zao zimeinuka juu! -
14 kuna kizazi ambacho meno yao ni upanga, na mifupa ya taya zao ni visu, ili waweze kumrarua masikini wamtoe duniani na mhitaji atoke miongoni mwa wanadamu.
15 Ruba anamabinti wawili, “Toa na Toa” wanalia. Kuna vitu vitatu ambavyo havitosheki, vinne ambavyo havisememi, “Inatosha”:
Mithali 30 in Biblia ya Kiswahili