Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 29:8-20 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 29:8-20 in Biblia ya Kiswahili

8 Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
9 Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
10 Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
11 Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
12 Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
13 Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
14 Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
15 Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
16 Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
17 Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
18 Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
19 Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
20 Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Mithali 29 in Biblia ya Kiswahili