1 Mithali za Sulemani mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.
2 Mithali hizi zinafundisha hekima na maarifa, kufundisha maneno ya busara,
3 ili mpate maarifa kwa ajili ya kuishi kwa kutenda wema, haki na adili.
4 Mithali hizi zinatoa hekima kwa wale ambao hawakufunzwa, na kuwapa vijana maarifa na hadhari.
5 Watu wenye busara wasikie na kuongeza elimu yao na watu wenye ufahamu wapate mwongozo,