Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 1:1-13 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 1:1-13 in Biblia ya Kiswahili

1 Mithali za Sulemani mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.
2 Mithali hizi zinafundisha hekima na maarifa, kufundisha maneno ya busara,
3 ili mpate maarifa kwa ajili ya kuishi kwa kutenda wema, haki na adili.
4 Mithali hizi zinatoa hekima kwa wale ambao hawakufunzwa, na kuwapa vijana maarifa na hadhari.
5 Watu wenye busara wasikie na kuongeza elimu yao na watu wenye ufahamu wapate mwongozo,
6 kwa kuelewa mithali, misemo, vitendawili na maneno ya wenye busara.
7 Hofu ya Yehova ni chanzo cha maarifa- wapumbavu hudharau hekima na nidhamu.
8 Mwanangu, sikia fundisho la baba yako na wala usiziache kanuni za mama yako;
9 zitakuwa kilemba cha neema katika kichwa chako na jebu zinazoning'inia kwenye shingo yako.
10 Mwanangu wenye dhambi wakikushawishi katika dhambi zao, kataa kuwafuata.
11 Kama watasema, “haya tufuatae, tuvizie ili kufanya mauaji, tujifiche ili tuwashambulie watu wasio na hatia, pasipo sababu.
12 Haya tuwameza wakiwa hai, kama kuzimu inavyowachukua wenye afya, na kuwa kama wale waangukao kwenye shimoni.
13 Tutapata vitu vyote vya thamani; tutazijaza nyumba zetu vile tunavyoiba kwa wengine.
Mithali 1 in Biblia ya Kiswahili