Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 16:18-30 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 16:18-30 in Biblia ya Kiswahili

18 Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
19 Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
20 Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
21 Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
Mithali 16 in Biblia ya Kiswahili