Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 12:12-23 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 12:12-23 in Biblia ya Kiswahili

12 Watu waovu hutamani wanavyoiba watu wabaya kutoka kwa wengine, bali tunda la wale watendao haki hutoka kwao mwenyewe.
13 Mtu mbaya hunaswa kwa maongezi yake mabaya, bali wale watendao haki hujinasua katika taabu.
14 Mtu hushiba vitu vyema kutokana na tunda la maneno yake, kama vile kazi ya mikono yake inavyompa thawabu.
15 Njia ya mpumbavu ni sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu wa hekima husikiliza ushauri.
16 Mpumbavu huonyesha hasira yake papo hapo, bali asiyejali tusi ni mwenye busara.
17 Asemaye ukweli huongea ilivyo haki, bali shahidi wa uongo huongea uongo.
18 Maneno yake asemaye kwa pupa ni kama kurusha upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
19 Midomo yenye kweli itadumu milele, bali ulimi wa uongo ni kwa kitambo kidogo tu.
20 Kuna udanganyifu katika mioyo ya wale wanaopanga kutenda uovu, bali furaha hutoka kwa washauri wa amani.
21 Hakuna ugonjwa utakaowajia wale watendao haki, bali watu waovu watajazwa matatizo.
22 Yehova anachukia midomo ya uongo, bali wale ambao huishi kwa uaminifu ndiyo furaha yake.
23 Mtu mwenye busara anasitiri maarifa yake, bali moyo wa wapumbavu hupiga yowe za kipumbavu.
Mithali 12 in Biblia ya Kiswahili