Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 11:20-30 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 11:20-30 in Biblia ya Kiswahili

20 Yehova anawachukia wenye ukaidi mioyoni, bali anawapenda wale ambao njia zao hazina makosa.
21 Uwe na uhakika juu ya hili- watu waovu hawatakosa adhabu, bali uzao wa wale watendao haki watawekwa salama.
22 Kama pete ya dhahabu kwenye pua ya nguruwe ndiyo alivyo mwanamke mzuri asiye na busara.
23 Shauku ya wale watendao haki ni matokeo mema, bali watu waovu wanaweza kutumainia ghadhabu tu.
24 Kuna yule ambaye hupanda mbegu- atakusanya zaidi; mwingine hapandi- huyo anakuwa masikini.
25 Mtu mkarimu atafanikiwa na yule awapaye maji wengine atapata maji yake mwenyewe.
26 Watu wanamlaani mtu ambaye hukataa kuuza nafaka, bali zawadi njema hufunika kichwa chake ambaye huuza nafaka.
27 Yule ambaye hutafuta mema kwa bidii pia anatafuta kibali, bali yule atafutaye ubaya atapata ubaya.
28 Wale wanaotumaini utajiri wataanguka, bali kama jani, wale watendao haki watasitawi.
29 Yule ambaye analeta taabu kwenye kaya yake ataurithi upepo na mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye moyo wa hekima.
30 Wale watendao haki watakuwa kama mti wa uzima, lakini vurugu huondoa uzima.
Mithali 11 in Biblia ya Kiswahili