Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mhubiri 3:6-11 in Swahili (individual language)

Help us?

Mhubiri 3:6-11 in Biblia ya Kiswahili

6 Kuna wakati wa kutafuta vitu na wakati wa kutotafuta, wakati wa kutunza vitu na wakati wa kuvitupa,
7 wakati kuchana mavazi na wakati wa kuyashona, wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza.
8 Kuna wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.
9 Ni faida gani mfanyakazi aipatayo katika kazi yake?
10 Nimeona kazi ambayo Mungu amewapa wanadamu kuitimiza.
11 Mungu amefanya kila kitu kufaa kwa wakati wake. Pia ameweka umilele ndani ya mioyo yao. Lakini mwanadamu hawezi kuelewa matendo ambayo Mungu ameyafanya, tangu mwanzo wao hadi mwisho.
Mhubiri 3 in Biblia ya Kiswahili