Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Marko - Marko 8

Marko 8:13-23

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13Kisha akawaacha, akaingia ndani ya mashua tena, akaondoka kuelekea upande mwingine.
14Wakati huo wanafunzi walisahau kuchukua mikate. Hawakuwa na mikate zaidi ya kipande kimoja kilichokuwa kwenye mashua.
15Aliwaonya na kusema, “Muwe macho na mjilinde dhidi ya chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.
16Wanafunzi wakasemezana wao kwa wao, “Ni kwa sababu hatuna mikate.”
17Yesu alilitambua hili, na akawaambia, “Kwa nini mnasemezana kuhusu kutokuwa na mikate? Hamjajua bado? Hamuelewi? Mioyo yenu imekuwa miepesi?
18Mna macho, hamuoni? Mna masikio, hamsikii? Hamkumbuki?
19Nilipoigawanya mikate mitano kwa watu elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate?” Wakamjibu, “kumi na mbili.”
20“Na nilipoigawanya mikate saba kwa watu elfu nne, mlichukua vikapu vingapi?”
21Wakasema, “Saba.” Akawaambia, “Bado hamuelewi?”
22Wakaja Bethsaida. Watu hao walimleta kwa Yesu mtu kipofu na wakamsihi Yesu amguse.
23Yesu akamshika kwa mkono yule kipofu, na kumwongoza nje ya kijiji. Alipotema mate juu ya macho yake na kunyosha mikono yake juu yake, alimuuliza, “Unaona chochote?”

Read Marko 8Marko 8
Compare Marko 8:13-23Marko 8:13-23