Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mambo ya Walawi 8:5-9 in Swahili (individual language)

Help us?

Mambo ya Walawi 8:5-9 in Biblia ya Kiswahili

5 “Hivi ndivyo alivyotuamru Yahweh tutende.”
6 Musa akamleta Aroni na wanawe na kuwaosha kwa maji.
7 Akamvika Aroni kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini na kumfunga ukumbuu kiunoni mwake, akamvika joho la nje lenye mikono mirefu na kumvika kile kizibao chenye vipande viwili tumboni na mgongoni na kukifunga kuzunguka kiunoni mwake kwa mshipi uliosokotwa kwa ustadi na kukikaza mwilini mwake.
8 Kisha Musa akaweka kifuko kifuani mwa Aroni, na ndani ya kifuko hicho akaweka Urimu na Thumimu.
9 Na kisha akamfunga kiremba kichwani, na juu ya kiremba kwa mbele, akaweka bamba la dhahabu; liwe taji takatifu, kama Yahweh alivyomwamru yeye.
Mambo ya Walawi 8 in Biblia ya Kiswahili