Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mambo ya Walawi 21:11-18 in Swahili (individual language)

Help us?

Mambo ya Walawi 21:11-18 in Biblia ya Kiswahili

11 Hataingia kamwe mahali popote ambapo kuna maiti na kujitia unajisi, hata kama ni maiti ya baba yake au ya mama yake.
12 Kuhani mkuu hataondoka eneo takatifu la hema la kukutania au kupatia unajisi patakatifu pa Mungu wake, kwa sababu amewekwa wakfu kuwa kuhani mkuu kwa kutiwa mafuta ya upako ya Mungu wake. Mimi ndimi Yahweh.
13 Kuhani mkuu nilazima aoe bikira kuwa mke wake.
14 Hataoa mjene, mwanamke mtalaka au mwanamke aliye kahaba. Anaweza kuoa mwanamke bikira kutoka kwa watu wake,
15 kwa hiyo asiwatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake. kwa kuwa Mimi Yahweh, ndimi ninayemfanya yeye mtakatifu.”
16 Yahweh akamwambia Musa, akasema,
17 Zungumza na Aroni na umwambie, 'mtu yeyote wa ukoo wako katika vizazi vyako vyote mwenye kasoro mwilini mwake, asisogee kutoa chakula kwa Mungu wake.
18 Mtu yeyote mwenye kasoro mwilini mwake asimkaribie Yahweh,
Mambo ya Walawi 21 in Biblia ya Kiswahili