Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mambo ya Walawi 18:4-15 in Swahili (individual language)

Help us?

Mambo ya Walawi 18:4-15 in Biblia ya Kiswahili

4 Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
5 Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
6 Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
7 Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
8 Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
9 Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
10 Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
11 Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
12 Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
13 Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
14 Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
15 Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
Mambo ya Walawi 18 in Biblia ya Kiswahili