Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mambo ya Walawi 18:11-19 in Swahili (individual language)

Help us?

Mambo ya Walawi 18:11-19 in Biblia ya Kiswahili

11 Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
12 Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
13 Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
14 Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
15 Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
16 Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
17 Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
18 Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
19 Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
Mambo ya Walawi 18 in Biblia ya Kiswahili