Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mambo ya Walawi 11:27-30 in Swahili (individual language)

Help us?

Mambo ya Walawi 11:27-30 in Biblia ya Kiswahili

27 Mnyama yeyote anayetembea kwa vitanga vyake miongoni mwa wanyama waendao kwa miguu yote minne ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mzoga kama huo atakuwa najisi hata jioni.
28 Na yeyote aokotaye mzoga kama huo ni zazima atazifua nguo zake na kuwa najisi hata jioni. Wanyama hawa watakuwa najisi kwenu.
29 Kuhusiana na wanyama wataambaao juu ya ardhi, hawa ndiyo walio najisi kwenu: kicheche, panya, aina zote za mijusi mikubwa, guruguru,
30 kenge, mijusi ya ukutani, goromoe, na kinyonga.
Mambo ya Walawi 11 in Biblia ya Kiswahili