Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Luka - Luka 19

Luka 19:14-24

Help us?
Click on verse(s) to share them!
14Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
15Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
16Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi.'
17Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi.'
18Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
19Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
20Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
21kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda.'
22Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
23Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
24Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'

Read Luka 19Luka 19
Compare Luka 19:14-24Luka 19:14-24