Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Hesabu 10:22-33 in Swahili (individual language)

Help us?

Hesabu 10:22-33 in Biblia ya Kiswahili

22 Majeshi ya kabila la uzao wa Efraimu ndio waliofuata. Elishama mwana wa Amihudi ndiye aliyeongoza jeshi la Efraimu.
23 Gamalieli mwana wa Pedazuri aliongoza jeshi la uzao wa Manase.
24 Abidani mwana wa Gidioni aliongoza jeshi la uzao wa kabila la Benjamini.
25 Lile jeshi lililoweka kambi mahali pa bango la uzao wa Dani lilikuwa la mwisho kuondoka. Ahizeri mwana wa Amishadai ndiye aliyeongoza jeshi la Dani.
26 Pagieli mwana wa Okirani aliongoza jeshi la wana wa uzao wa Asheri.
27 Ahira mwana wa Enani aliongoza jeshi la uzao wa kabila ya Naftali.
28 Hivi ndivyo majeshi ya wana wa Israeli yalivyosafiri.
29 Musa alinena na Hobibu mwana wa Reueli wa Kabila la Midiani. Reueli alikuwa baba mke wa Musa. Musa akanena na Hobibu akasema, “Tunasafiri kuelekea mahali ambapo BWANA ametuahidi. BWANA alisema kuwa, “Nitawapeni ninyi hilo eneo, 'Njoni pamoja nasi na tutawatendea mema. BWANA ameahidi kuwafanyia mema Waisraeli.”
30 Lakini Hobibu akmwambia Musa, “Sitaambatana nanyi.”
31 Naye Musa akamjibu, “Tafadhali msituache. Mnajua jinsi ilivyo kuweka kambi jangwani. Tunaomba mtujali.
32 Kama mtaambatana nasi tutawatendea mema sawa na jinsi BWANA anavyotutendea.”
33 Walisafiri kutoka mlima wa BWANA kwa siku tatu. Sanduku la agano la BWANA liliwatangulia kwa siku tatu ili kupata mahali pa kupumzika.
Hesabu 10 in Biblia ya Kiswahili