Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Hesabu 10:11-20 in Swahili (individual language)

Help us?

Hesabu 10:11-20 in Biblia ya Kiswahili

11 Katika siku ya ishrini, mwezi wa pili, mwaka wa pili, Lile wingu liliinuliwa toka masikani ya amri za maagano.
12 Wana wa Israeli wakaendelea na safari yao toka jangwa la Sinai. Lile wingu likasimama kwenye jangwa la Parani.
13 Walifanya safari yao ya kwanza, kufuatia amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa.
14 Kambi ya mahali pa uzao wa Yuda iliondoka ya kanza, wakiondoa majeshi yao binafsi. Nashoni mwana wa Aminadabu ndiye aliyeongoza jeshi la Yuda.
15 Nethaneli mwana wa Zuari aliongoza jeshi la kabila la uzao wa Isakari.
16 Eliabu mwana wa Heloni aliongoza jeshi la kabila la Zabuloni.
17 Uzao wa Gerishoni na Merari, ambao walitunza masikani, na kuanza kusafiri.
18 Baadaye Walifuata jeshi la mahali pa kambi ya Reubeni walianza safari yao. Elizuri mwana wa Shedeuri alliongoza jeshi la Reubebni.
19 Shelumieli mwana wa Zurishadai aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Simeoni.
20 Eliasafu mwana Deuli aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Gadi.
Hesabu 10 in Biblia ya Kiswahili