1Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya; mwimbieni Yahwe, nchi yote.
2Mwimbieni Yahwe, tukuzeni jina lake; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
3Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, matendo yake ya ajabu kati ya mataifa.
4Maana Yahwe ni mkuu na wakusifiwa sana. Ni wakuhofiwa kuliko miungu mingine.
5Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.