Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 95

Zaburi 95:2-8

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2Tuingie uweponi mwake kwa shukrani; tumwimbie yeye kwa zaburi ya sifa.
3Kwa maana Yahwe ni Mungu mkuu na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4Mkononi mwake zimo bonde za dunia; navyo vilele vya milima ni vyake.
5Bahari ni yake, maana aliiumba, na mikono yake ilitengeneza nchi kavu.
6Oh njoni, tumwabudu na tupige magoti; tupige magoti mbele za Yahwe, muumbaji wetu:
7Kwa maana yeye ni Mungu wetu, na sisi tu watu wa malisho yake na kondoo wa mkono wake. Ni heri leo mngesikia sauti yake!
8Msiifanye migumu mioyo yenu, kama vile huko Meriba, au kama ile siku ya Masa jangwani,

Read Zaburi 95Zaburi 95
Compare Zaburi 95:2-8Zaburi 95:2-8