6Mtu mpumbavu hawezi kuyajua, wala mjinga kuyaelewa haya:
7Wasio haki watakapochipuka kama nyasi, na hata watendao uovu watakapo stawi, bado wataangamizwa kwenye uharibifu wa milele.
8Lakini wewe, Yahwe, utatawala milele.
9Hakika, watazame adui zako, Yahwe! Hakika, watazame adui zako. Wataangamia! Wale wote watendao maovu watatawanywa.
10Wewe umeyainua mapembe yangu kama mapembe ya Nyati wa porini; nimepakwa mafuta safi.
11Macho yangu yameona kuanguka kwa adui zangu; masikio yangu yamesikia maangamizi ya maadui zangu waovu.
12Wenye haki watastawi kama mtende; watakua kama mwerezi wa Lebanoni.