Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 91

Zaburi 91:1-9

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
2Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
3Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
4Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
5Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
6wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
7Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
8Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
9Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.

Read Zaburi 91Zaburi 91
Compare Zaburi 91:1-9Zaburi 91:1-9