Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 89

Zaburi 89:38-45

Help us?
Click on verse(s) to share them!
38Lakini wewe umemtupa na kumkataa; umemkasirikia mfalme mpakwa mafuta wako.
39Wewe umelikataa agano la mtumishi wako. Umeinajisi taji yake ardhini.
40Umevunja kuta zake zote. Umeharibu ngome yake.
41Wapita njia wote wamemuibia, amekuwa kitu chenye kinyaa kwa majirani zake.
42Umeinua mkono wa kuume wa adui zake; umewafurahisha adui zake wote.
43Umeyageuza makali ya upanga wake. Na hukumfanya asimame awapo vitani.
44Umeimaliza fahari yake; umekitupa ardhini kiti chake cha enzi.
45Umefupisha siku za ujana wake. Umemfunika kwa aibu. Selah

Read Zaburi 89Zaburi 89
Compare Zaburi 89:38-45Zaburi 89:38-45