34Sitavunja agano langu wala kubadilisha maneno ya midomoni mwangu.
35Mara moja na kwa yote, nimeapa kwa utakatifu wangu sitamdanganya Daudi:
36uzao wake utaendelea milele na kiti chake cha enzi kama vile jua mbele yangu.
37Kitaimarishwa milele kama mwezi, shahidi mwaminifu mawinguni.” Selah
38Lakini wewe umemtupa na kumkataa; umemkasirikia mfalme mpakwa mafuta wako.
39Wewe umelikataa agano la mtumishi wako. Umeinajisi taji yake ardhini.