Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 89

Zaburi 89:29-44

Help us?
Click on verse(s) to share them!
29Nitaufanya uzao wake kudumu milele na kiti chake cha enzi kitadumu kama mbingu zilizo juu.
30Ikiwa watoto wake wataziacha sheria zangu na kutokutii amri zangu,
31na kama watazivunja sheria zangu na kutokuzishika amri zangu,
32ndipo nitauadhiu uasi wao kwa fimbo na uovu wao kwa makofi.
33Lakini sitauondoa kwake upendo wangu thabiti wala kutokuwa mwaminifu kwa ahadi yangu.
34Sitavunja agano langu wala kubadilisha maneno ya midomoni mwangu.
35Mara moja na kwa yote, nimeapa kwa utakatifu wangu sitamdanganya Daudi:
36uzao wake utaendelea milele na kiti chake cha enzi kama vile jua mbele yangu.
37Kitaimarishwa milele kama mwezi, shahidi mwaminifu mawinguni.” Selah
38Lakini wewe umemtupa na kumkataa; umemkasirikia mfalme mpakwa mafuta wako.
39Wewe umelikataa agano la mtumishi wako. Umeinajisi taji yake ardhini.
40Umevunja kuta zake zote. Umeharibu ngome yake.
41Wapita njia wote wamemuibia, amekuwa kitu chenye kinyaa kwa majirani zake.
42Umeinua mkono wa kuume wa adui zake; umewafurahisha adui zake wote.
43Umeyageuza makali ya upanga wake. Na hukumfanya asimame awapo vitani.
44Umeimaliza fahari yake; umekitupa ardhini kiti chake cha enzi.

Read Zaburi 89Zaburi 89
Compare Zaburi 89:29-44Zaburi 89:29-44