Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 89

Zaburi 89:23-33

Help us?
Click on verse(s) to share them!
23Nitawaangamiza adui zake mbele yake; nitawaua wale wamchukiao.
24Kweli yangu na uaminifu wa agano vitakuwa pamoja naye; kupitia jina langu atakuwa mshindi.
25Nitaweka mkono wake juu ya bahari na mkono wake wa kuume juu ya mito.
26Yeye ataniita, 'Wewe ni Baba yangu, Mungu wangu, na mwamba wa wokovu wangu.'
27Nitamjalia kuwa kama mzaliwa wangu wa kwanza, aliye inuliwa zaidi juu ya wafalme wa nchi.
28Nitaongeza uaminifu wa agano langu kwake milele; na agano langu pamoja naye litakuwa salama.
29Nitaufanya uzao wake kudumu milele na kiti chake cha enzi kitadumu kama mbingu zilizo juu.
30Ikiwa watoto wake wataziacha sheria zangu na kutokutii amri zangu,
31na kama watazivunja sheria zangu na kutokuzishika amri zangu,
32ndipo nitauadhiu uasi wao kwa fimbo na uovu wao kwa makofi.
33Lakini sitauondoa kwake upendo wangu thabiti wala kutokuwa mwaminifu kwa ahadi yangu.

Read Zaburi 89Zaburi 89
Compare Zaburi 89:23-33Zaburi 89:23-33