3Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni.
4Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
5Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
6Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.