Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 85

Zaburi 85:2-10

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. Selah
3Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
4Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
5Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
6Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
7Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
8Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
9Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
10Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.

Read Zaburi 85Zaburi 85
Compare Zaburi 85:2-10Zaburi 85:2-10