1Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
2Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. Selah
3Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
4Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
5Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
6Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.