Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 81

Zaburi 81:6-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
6“Niliutua mzigo kutoka mabegani mwake; mikono yake ilipumzishwa kubeba kikapu.
7Katika dhiki yako uliniita, nami nikakusaidia; nilikujibu kutoka katika wingu jeusi la radi. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba. Selah
8Sikilizeni, watu wangu, nami nitawaonya, Israeli, kama tu ugalinisikiliza!
9Lazima kati yenu kusiwepo na mungu wa kigeni; haupaswi kumwabudu mungu wa kigeni.
10Mimi ni Yahwe niliyekutoa katika nchi ya Misri, fungua sana kinywa chako, nami nitakijaza.
11Lakini watu wangu hawakusikiliza maneno yangu; Israeli hawakunitii.
12Nikawaacha waende katika katika njia yao wenyewe ya ukaidi ili kwamba waweze kufanya kinachoonekana sahihi kwao.
13Oh, laiti watu wangu wangenisikiliza mimi; oh, watu wangu wangelitembea katika njia yangu.
14Kisha ningewatiisha adui zao haraka na kugeuzia mkono wangu dhidi ya watesi wao.
15Wale wanaomchukia Yahwe katika hofu na waanguke chini mbele zake! Wawe wanyonge milele.
16Ningewalisha Israeli kwa ngano bora; Ningewatosheleza kwa asali itokayo mwambani.”

Read Zaburi 81Zaburi 81
Compare Zaburi 81:6-16Zaburi 81:6-16