67Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.