Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 78

Zaburi 78:56-72

Help us?
Click on verse(s) to share them!
56Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.

Read Zaburi 78Zaburi 78
Compare Zaburi 78:56-72Zaburi 78:56-72