Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 78

Zaburi 78:20-35

Help us?
Click on verse(s) to share them!
20Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.

Read Zaburi 78Zaburi 78
Compare Zaburi 78:20-35Zaburi 78:20-35