Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 77

Zaburi 77:8-20

Help us?
Click on verse(s) to share them!
8Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? Selah
10Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
14Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
15Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. Selah
16Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
17Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
18Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
19Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
20Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.

Read Zaburi 77Zaburi 77
Compare Zaburi 77:8-20Zaburi 77:8-20