5Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
6Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
7Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? Selah