Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 77

Zaburi 77:10-17

Help us?
Click on verse(s) to share them!
10Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
14Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
15Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. Selah
16Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
17Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.

Read Zaburi 77Zaburi 77
Compare Zaburi 77:10-17Zaburi 77:10-17