Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 74

Zaburi 74:3-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Uje utazame uharibifu kamili, uharibifu ambao umefanywa na adui mahali patakatifu.
4Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
5Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
6Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
7Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
8Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
9Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
10Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
11Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
12Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
13Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
14Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
15Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
16Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
17Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.
18Kumbula vile adui alivyo vurumisha matusi kwako, Yahwe, na kwamba watu wapumbavu wamelitukana jina lako.

Read Zaburi 74Zaburi 74
Compare Zaburi 74:3-18Zaburi 74:3-18