12Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
13Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
14Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
15Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
16Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
17Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.