Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 73

Zaburi 73:5-23

Help us?
Click on verse(s) to share them!
5Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
11Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.

Read Zaburi 73Zaburi 73
Compare Zaburi 73:5-23Zaburi 73:5-23