4Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
5Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.