19Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.